Luka 12:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
28 Basi ikiwa Mungu anavalisha majani kama hivi, yanayoonekana pale leo na kesho yanatoweka na kutupwa, hatawavalisha vizuri zaidi ninyi wenye imani ndogo?
Na Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka. Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”
Yesu akawajibu: “Kwa sababu imani yenu ni ndogo. Kweli ninawaambia kama mukiwa na imani, hata ikiwa tu kama punje ndogo sana ya mbegu ya haradali, mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Toka hapa uende kule,’ nao utatoka pale. Hakuna kitu chochote kitakachokosa kuwezekana kwenu. [
Basi ikiwa Mungu anavalisha majani kama hivi, yanayoonekana leo na kesho yanatoweka na kutupwa katika moto, hatawavalisha ninyi vizuri zaidi, ninyi wenye imani ndogo?
Yesu akawajibu: “Sababu gani munaogopa kama hivi? Hakika imani yenu ni ndogo!” Halafu akasimama, akakaripia zoruba na maji na kukakuwa kimya kabisa ndani ya ziwa.
Halafu akawaambia wanafunzi wake: “Imani yenu iko wapi?” Nao wakaogopa na kushangaa, wakiulizana: “Huyu ni mutu gani? Anaamuru hata zoruba na ziwa, navyo vinamutii!”