Luka 12:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
19 Kisha nitajisemesha hivi juu yangu mwenyewe: ‘Uko na mali nyingi ulizoweka akiba kwa miaka mingi. Sasa utulizane, ukule na kunywa na kujifurahisha.’
Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.
Lakini ninyi mukafurahi na kusherehekea. Mulichinja ngombe na kondoo, mukakula nyama na kunywa divai. Ninyi mulisema: Acha tukule na kunywa maana kesho tutakufa.
Ole kwao wanaoongeza nyumba juu ya nyumba, wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao, mpaka kila sehemu inakuwa mali yao, na hakuna nafasi kwa wengine katika inchi.
“Mujilinde vizuri, kusudi musilemewe na kutafuta kula ulafi, kulewa na kusumbukia maisha. Kama si vile, Siku ile ya kurudia kwa Kristo itawafikia kwa rafla
Ikiwa ni kwa nia ya kimutu, nimepigana na nyama wakali wa pori katika Efeso, jambo lile limenifalia nini? Kama wafu hawafufuki, basi: “Tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.”
Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.
Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.
Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu.
Na kwa kadiri ulivyojitukuza na kuishi katika raha, kwa kadiri ile ile muuletee mateso na huzuni. Muji ule unajisemesha: ‘Mimi ninaikaa juu ya kiti cha kifalme kama vile malkia; mimi si mujane, wala sitapata huzuni hata kidogo!’
Yule kijana alimwongoza Daudi mpaka kwenye kundi lile. Walipofika kule waliwakuta wanyanganyi wale wakiwa wametawanyika kila pahali maana walikuwa wakikula na kunywa kwa sababu vitu walivyonyanganya kutoka inchi ya Wafilistini na inchi ya Yuda vilikuwa vingi sana.