Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 12:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Kisha nitajisemesha hivi juu yangu mwenyewe: ‘Uko na mali nyingi ulizoweka akiba kwa miaka mingi. Sasa utulizane, ukule na kunywa na kujifurahisha.’

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 12:19
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu anazaliwa na mwanamuke, ana siku chache, na taabu nyingi.


Maana atakapokufa hatachukua kitu chochote, mali yake haitashuka huko chini pamoja naye.


Wanadamu wote ni kama pumzi tu; wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu. Wakipimwa wote pamoja, pumzi ni nzito kuliko wao.


Mali iliyopatikana kwa njia mbaya haifai, lakini haki inaokoa mutu kutoka kifo.


Mali ni taji ya utukufu wa wenye hekima, lakini ujinga ni kitambaa cha wapumbafu.


Tajiri anazani kwamba mali ni makimbilio yake; anafikiri hayo ni ukuta murefu unaomulinda.


Macho yako yatakapokuwa yanaanza tu kuuona, nao utatoweka mara moja. Maana hakika utajiri unaota mabawa, unaruka na kutoweka katika anga kama tai.


Usijisifie kwa ajili ya kesho. Haujui siku ya leo itakuletea nini.


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Hakuna kitu kizuri kwa mwanadamu, isipokuwa kula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake. Hili nalo nimeliona kwamba linatoka kwa Mungu,


Lakini ninyi mukafurahi na kusherehekea. Mulichinja ngombe na kondoo, mukakula nyama na kunywa divai. Ninyi mulisema: Acha tukule na kunywa maana kesho tutakufa.


Ole kwao wanaoamuka asubui mapema wapate kukimbilia kinywaji cha kulewesha; wanaokesha hata usiku, mpaka divai iwaleweshe!


Ole kwao wanaoongeza nyumba juu ya nyumba, wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao, mpaka kila sehemu inakuwa mali yao, na hakuna nafasi kwa wengine katika inchi.


Wao wanaambiana hivi: Mukuje, tuende kutafuta divai; mukuje tukunywe tushibe kinywaji kikali! Kesho itakuwa kama leo, tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.


Efuraimu ni sawa na muchuuzi anayetumia vipimo vya udanganyifu, anayependa kudanganya watu.


Ninyi munashangilia juu ya muji wa Bure na kusema mumeuteka muji wa Nguvu kwa nguvu zenu wenyewe.


Kwa hiyo, wanazitambikia nyavu zao, na kuzifukizia ubani; maana kwa njia ya vitu hivyo mapato yao yanaongezeka, na wanakuwa na chakula kingi.


Kisha akajisemesha: ‘Nitafanya hivi: nitabomoa gala zangu na nitajenga zingine kubwa zaidi, na mule nitaweka mavuno yangu yote na mali zangu zingine.’


“Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyezoea kuvaa nguo zenye kuwa laini sana za bei kali zaidi na aliyeishi katika raha siku zote.


“Mujilinde vizuri, kusudi musilemewe na kutafuta kula ulafi, kulewa na kusumbukia maisha. Kama si vile, Siku ile ya kurudia kwa Kristo itawafikia kwa rafla


Ikiwa ni kwa nia ya kimutu, nimepigana na nyama wakali wa pori katika Efeso, jambo lile limenifalia nini? Kama wafu hawafufuki, basi: “Tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.”


Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.


Lakini mujane anayeishi katika tamaa mbaya amekwisha kufa, ijapokuwa angali bado muzima.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Watakuwa wenye kutoana, wenye kichwa kigumu, wenye majivuno na wenye kupenda tamaa ya vitu kuliko kumupenda Mungu.


Mumeishi katika utajiri na kujifurahisha katika maisha yenu katika dunia. Mumejinenepesha kwa kuwa tayari kwa siku ya kuchinjwa.


Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu.


Na kwa kadiri ulivyojitukuza na kuishi katika raha, kwa kadiri ile ile muuletee mateso na huzuni. Muji ule unajisemesha: ‘Mimi ninaikaa juu ya kiti cha kifalme kama vile malkia; mimi si mujane, wala sitapata huzuni hata kidogo!’


Yule kijana alimwongoza Daudi mpaka kwenye kundi lile. Walipofika kule waliwakuta wanyanganyi wale wakiwa wametawanyika kila pahali maana walikuwa wakikula na kunywa kwa sababu vitu walivyonyanganya kutoka inchi ya Wafilistini na inchi ya Yuda vilikuwa vingi sana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ