Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 12:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Yesu akamujibu: “Ewe bwana, ni nani aliyeniweka kuwa mwamuzi wenu au mutu wa kuwagawanyia mali zenu?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 12:14
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye akamujibu: “Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi wetu? Unataka kuniua kama vile ulivyomwua yule Mumisri?” Kwa hiyo, Musa akaogopa na kufikiri: “Bila shaka jambo hilo limejulikana!”


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Mutu mumoja katika kundi akamwambia Yesu: “Mwalimu, umwambie ndugu yangu anipe sehemu yangu ya urizi, baba aliotuachia.”


Nyuma kidogo mutu mwingine akamwona, na akasema: “Wewe vilevile ni mumoja wao!” Lakini Petro akamujibu mutu yule: “Mimi si mumoja wao.”


Yesu alipoona namna walivyomwaminia, akasema: “Rafiki yangu, zambi zako zimesamehewa.”


Wakati Yesu alipotambua kama walitaka kuja kumutwaa kwa nguvu na kumuweka kuwa mufalme, akaondoka na kwenda tena kwa kilima peke yake.


Mwanamuke yule akamujibu: “Bwana, hakuna mutu.” Basi Yesu akamwambia: “Mimi vilevile sikuhukumu. Ujiendee, lakini usifanye zambi tena.”]


Wewe unayemuhukumu mwingine hauna namna yoyote ya kujitetea, haizuru wewe ni nani. Kwa maana wakati unapohukumu mwingine, unajikatia hukumu wewe mwenyewe, kwa sababu wewe unayehukumu unatenda mambo yale yale.


Basi wewe unawahukumu wale wanaofanya mambo yale, lakini wewe mwenyewe unayafanya! Unafikiri kwamba utaponyoka hukumu ya Mungu?


Halafu sasa wewe mwanadamu ni nani hata ubishane na Mungu? Chombo cha udongo hakiwezi kumwuliza mufinyanzi: “Kwa nini umenitengeneza hivi?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ