Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.
Lakini munauliza: Kwa nini mutoto asiazibiwe kwa sababu ya zambi za baba yake? Mutoto akitenda mambo ya haki na ya ukweli, kama akiwa mwangalifu kushika masharti yangu yote, basi, huyo hakika ataishi.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munafanana na makaburi yaliyopakaliwa chokaa, yanayoonekana kuwa mazuri kwa inje, lakini ndani yanajaa mifupa ya wafu na uchafu wa kila namna.
Nao wanajua kwamba Sheria ya Mungu inasema kwamba watu wanaotenda maneno haya wanastahili kufa. Lakini hata hivi wanaendelea, si kuyafanya tu, lakini kukubaliana na wale wanaoyatenda.