Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 11:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Halafu Bwana akamwambia: “Ninyi Wafarisayo ni kama mutu anayesafisha tu inje ya kikombe na sahani; lakini ndani yenu mumejaa tamaa ya wizi na uovu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 11:39
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alipoona uwingi wa uovu wa watu katika dunia, na kwamba kila kitu mwanadamu anachokusudia ndani ya moyo wake ni kiovu siku zote,


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe ingawa hakutenda kwa moyo mukamilifu.


Waadui wengi wananizunguka kama ngombe dume; wamenisonga kama ngombe dume wanono wa Basani!


Kama vile rangi yenye kungaa iliyopakwa juu ya chungu cha udongo, ndivyo maneno matamu yenye nia mbaya yanavyokuwa.


Akisema maneno mazuri usimwaminie. Ndani ya moyo wake kuna machukizo mengi.


Kuna watu ambao wanajiona kuwa safi, kumbe bado hawajatakaswa uchafu wao.


Wewe Yerusalema, usafishe maovu ya moyo wako, kusudi upate kuokolewa. Mpaka wakati gani utaendelea kuchunga maovu?


Wakubwa wenu ni kama simba anayenguruma anaporarua nyama wake. Wanaua watu, wanawanyanganya watu mali na vitu vyao vya bei kali, na kuongeza hesabu ya wajane.


Wakubwa wake wanaokuwa ndani ya muji ni kama imbwa wa pori wanaorarua nyama wao; wanaua kwa kujitajirisha kwa namna isiyokuwa ya haki.


Wakubwa wake ni simba wanaonguruma, waamuzi wake ni imbwa wa pori wenye njaa magaribi wasioacha chochote mpaka asubui.


Kwa maana ndani ya moyo munatoka mawazo mabaya yanayoleta uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo na matukano.


“Mufanye angalisho na manabii wa uongo; kwa maana wanakuja kwenu wakionekana kwa inje kama vile kondoo, lakini ndani, wao ni kama imbwa wakali wa pori.


Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.


Bwana alipomwona yule mama, akamusikilia huruma na kumwambia: “Usilie.”


na kuwatuma kwa Bwana kumwuliza: “Wewe ndiwe yule aliyepaswa kuja kutuokoa au tumungojee mwingine?”


(Hakusema maneno haya kwa sababu aliwasikilia wamasikini huruma, lakini kwa sababu alikuwa mwizi. Ni yeye aliyekuwa akichunga mufuko wa feza, naye alikuwa akijitwalia mali toka ndani yake.)


Wakati Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakikula chakula cha magaribi, Shetani alikuwa amekwisha kumushawishi Yuda mwana wa Simoni Iskariota kwamba amutoe Yesu.


Basi Petro akamwuliza: “Anania, namna gani Shetani amekuingia hata akakusemesha uongo mbele ya Roho Mutakatifu na kuficha sehemu ya feza ulizopata ulipouzisha lile shamba?


Nami niliendelea vizuri sana katika dini ya Kiyuda kuwapita watu wote wengine wa kabila langu wenye umri wangu, nikijikaza sana kushika desturi za babu zetu.


Kwa inje watajionyesha kama watu wenye kushikamana na ibada, lakini wanazarau uwezo wake. Ujiepushe na watu hao.


Kila kitu ni safi kwa watu wanaokuwa safi. Lakini hakuna chochote kinachokuwa safi kwa watu wachafu na wasiomwamini Mungu, kwa maana akili na zamiri zao zimekuwa chafu.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ