Malkia wa Seba aliposikia sifa za Solomono, basi akafika Yerusalema kwa kumujaribu Solomono kwa maulizo magumu. Alifika Yerusalema akisindikizwa na watu wengi sana, pamoja na ngamia waliobeba marasi, zahabu nyingi sana na mawe ya bei kali. Na alipofika kwa Solomono, akamwuliza maulizo yote aliyokuwa nayo ndani ya moyo wake.