Luka 11:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
22 Lakini mutu mwingine mwenye nguvu zaidi akimushambulia na kumushinda, anamunyanganya silaha zake alizotegemea na kugawanya vitu vya unyanganyi anavyokuwa navyo.
Siku hiyo, Yawe atakamata upanga wake mukubwa, mukali na imara, na kuiazibu Leviatani, ile nyoka inayoruka na kuzongazonga. Yawe ataua nyoka mukubwa anayeishi katika bahari.
Kwa hiyo nitamugawanyia sehemu pamoja na wakubwa, atagawanya vitu vilivyotekwa pamoja na wenye nguvu. Alijitoa yeye mwenyewe hata kufa; aliwekwa kundi moja na watu wakosaji. Alizibeba zambi za watu wengi, akawaombea musamaha hao wakosaji.
Kwa hiyo sasa mutwae silaha zote Mungu anazowapatia. Kwa njia hii mutaweza kushinda adui yenu siku mbaya itakapowafikia. Nanyi mutakapokwisha kumaliza mapigano, mutaweza kusimama imara.
Mungu alinyanganya uwezo wa wakubwa na wenye mamlaka, naye akawaonyesha waziwazi, akiwatembeza kama wafungwa katika maandamano ya ushindi wa Mwana wake.
Mutu anayefanya zambi ni mutu wa Shetani, kwa maana Shetani anafanya zambi tangia mwanzo wa vitu vyote. Kwa sababu hii, Mwana wa Mungu alikuja kusudi aharibu kazi za Shetani.
Lakini ninyi, watoto wangu, muko watoto wa Mungu, nanyi mumewashinda manabii wa uongo; maana roho anayekaa ndani yenu ni mwenye uwezo kuliko yule anayekaa ndani ya watu wa dunia.