Lakini inatosha kwa mwanafunzi kufanana na mwalimu wake na mutumishi kufanana na bwana wake. Ikiwa wanamwita mukubwa wa jamaa Belzebuli, hawatakosa kuwaita watu wa jamaa yake kwa majina mabaya zaidi.
Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.
Halafu Wayuda wakamwambia: “Sasa tunajua hakika kwamba uko na pepo! Abrahamu amekufa, na manabii wamekufa vilevile, nawe unasema kwamba mutu akishika maneno yako, hatakufa hata milele.