10 Kwa maana kila mutu anayeomba anapewa; anayetafuta anapata, anayepiga hodi anafunguliwa mulango.
Yawe asifiwe, maana amenionyesha wema wake wa ajabu, nilipozungukwa katika muji unaoshambuliwa.
Nimewaza: Nimekata tamaa kabisa, tumaini langu kwa Yawe limetoweka.
Ingawa ninaita na kuomba musaada anazuiza maombi yangu yasimufikie.
Mutu akikuomba kitu, umupe. Na mutu akitaka umukopeshe, usimugeuzie mugongo.
Kwa maana kila mutu anayeomba, anapewa; naye anayetafuta, anapata, naye anayepiga hodi, anafunguliwa.
Ni baba gani kati yenu anaweza kumupa mutoto wake nyoka kama akimwomba samaki?
Nami ninawaambia: muombe nanyi mutapewa; mutafute nanyi mutapata; mupige hodi nanyi mutafunguliwa mulango.
Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu kwa kuwaonyesha kwamba wanapaswa kuomba siku zote pasipo kuchoka.
Wakati munapoomba, hamupati kitu kwa sababu munaomba kwa nia mbaya, kwa maana munataka vitu kusudi mutimize tu tamaa zenu.
Tunawaita watu hao kuwa wenye heri, kwa sababu walivumilia. Mumekwisha kusikia habari za uvumilivu wa Yobu, na munajua namna Bwana alivyomutendea kwa mwisho. Maana Bwana anajaa huruma na wema.