Luka 10:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
7 Mukae ndani ya nyumba ile, nanyi mukule na kunywa chochote watakachowapa, kwa maana mutumishi anastahili kupewa mushahara wake. Musihame nyumba kwa nyumba.
Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.
Kisha akapeleka Paulo na Sila ndani ya nyumba yake na kuwapatia chakula. Yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake walifurahi sana kwa sababu wamemwamini Mungu.
Huko mutafurahi mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi kati yenu kwa sababu hawana sehemu wala urizi kati yenu.
Na zaidi ya hiyo, wanashikwa na uvivu na kuwa na tabia ya kutangatanga nyumba kwa nyumba. Na si ile tu, vilevile wao ni wakatetea na wenye kujiingiza katika maneno ya watu wengine na kusema maneno yasiyofaa.