5 Na katika nyumba yoyote mutakapoingia, mutoe kwanza salamu mukisema: ‘Amani ikuwe katika nyumba hii!’
Mimi nitawapa amani, amani kwa wanaokuwa mbali na wanaokuwa karibu! –Ni Yawe anayesema hivyo.– Mimi nitawaponyesha.
Musibebe feza, wala mufuko, wala viatu, na musimusalimie mutu katika njia.
Kama mule mukiwa mutu anayekuwa tayari kupokea amani, atakaa na amani ile muliyomutakia. Kama si vile, amani ile itawarudilia.
Yesu akamwambia: “Leo nyumba hii imeokolewa, kwa sababu mutu huyu vilevile ni wa uzao wa Abrahamu.
Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.
Hivi, Kristo amekuja kutangaza Habari Njema ya amani kwa ninyi watu wa mataifa mengine, muliokuwa mbali na Mungu, na kwa Wayuda waliokuwa karibu naye.
Mutamwambia kwamba Daudi anakusalimia hivi: ‘Amani ikuwe kwako, kwa jamaa yako na yote unayokuwa nayo.