Ukawaonya kusudi warudilie Sheria yako, hata hivyo, kwa kiburi chao, wakaacha kutii amri zako. Wakaasi maagizo yako, ambayo kwa njia yake mutu akiyatii, ataishi. Wakakuwa wenye kiburi vilevile wakakuwa wagumu, na wakakataa kuwa watiifu.
Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.
Lakini hata wazao wao hao waliniasi. Hawakufuata masharti yangu, hawakushika wala kutimiza maagizo yangu ambayo mutu akiyashika, ataishi. Walizikufuru Sabato zangu. Basi nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuitimiza hasira yangu juu yao kule katika jangwa.
Yesu akamujibu: “Sababu gani unaniuliza juu ya jambo linalokuwa jema? Kuna mumoja tu anayekuwa mwema. Kama ukitaka kuingia pahali utakapopata uzima wa kweli, utii amri za Mungu.”
Yesu alipoona kwamba amejibu kwa akili, akamwambia: “Si mbali kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu.” Kisha maneno hayo hakuna mutu aliyesubutu tena kumwuliza Yesu neno.
Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.