Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 10:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 “Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 10:22
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


kama vile Baba anavyonijua mimi, na mimi ninavyomujua Baba. Vilevile mimi ninatoa maisha yangu kwa ajili ya kondoo wangu.


Yesu alijua kwamba Baba yake ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye mwenyewe alitoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.


Na yote ninayokuwa nayo ni yako, na yote unayokuwa nayo ni yangu, nami nimetukuzwa kwa njia yao.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Nimekujulisha kwao, na nitaendelea kukujulisha kusudi upendo ule unaokuwa nao kwangu ukuwe ndani yao, nami mwenyewe nikuwe ndani yao.”


Na sasa, Baba, unipe utukufu karibu nawe, utukufu unaokuwa sawa na ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuumbwa kwa dunia.


Baba anamupenda Mwana wake, naye ameweka vitu vyote kwa mukono wake.


Na nyuma ya pale, mwisho wa vyote utatimia. Wakati ule Kristo ataharibu utawala wote, mamlaka yote na uwezo wote, naye atamupatia Mungu Baba ufalme.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Na kule anatawala juu ya wakubwa wote, wenye mamlaka wote, wenye uwezo wote na wasultani wote na juu ya kila cheo kinachoweza kuwa katika dunia hii na katika dunia itakayokuja.


Umemupa mamlaka juu ya vitu vyote.” Wakati inaposemwa ya kama Mungu amemupa mutu mamlaka juu ya vitu vyote, maana yake hakuacha hata kitu kimoja. Ingawa hivi, hata sasa hatuoni kwamba amepewa mamlaka juu ya vitu vyote.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


Kila mutu atakayeenda mbali na asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, mutu yule hashirikiani na Mungu. Lakini yule anayedumu katika mafundisho yale, anashirikiana na Baba na Mwana vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ