Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 10:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Nawe muji Kapernaumu, unafikiri kwamba utapandishwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka chini katika kuzimu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 10:15
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakasema: “Tujijengee muji na munara ambao chongo yake itafika mbinguni kusudi tujipatie sifa, kusudi tusisambazwe katika dunia yote.”


Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa, imepanua kinywa chake mpaka mwisho. Waheshimiwa pamoja na watu wengine wa Yerusalema wanaingia humo makundi kwa makundi, vilevile na wote wanaushangilia kwa furaha.


Ingawa Babeli ungepanda mpaka mbinguni, na kuziimarisha kuta zake ndefu, waangamizaji watakuja kutoka kwangu kwa kuuharibu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitakuteremusha ndani ya shimo kusudi ujiunge na wale wanaokuwa huko, walioishi zamani katika dunia; utakaa kule katika matongo kwa milele. Hautakaliwa na watu milele na hautakuwa na nafasi katika inchi za wanaokuwa wazima.


Kwa uzuri na ukubwa wa muti huo, hakuna muti wowote katika bustani ya Edeni ambao uliweza kulinganishwa nao. Sasa, muti huo ni wewe Mufalme wa Misri. Wewe utatupwa chini kwa wafu pamoja na miti ya Edeni. Utalala karibu na wale wasiomujua Mungu na wale waliouawa kwa upanga. Hiyo itakuwa hali yako ewe Mufalme wa Misri, wewe na watu wako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Wewe mwanadamu! Uwaombolezee watu wengi wa Misri. Uwapeleke chini kwenye inchi ya wafu pamoja na mataifa mengine yenye nguvu, waende huko pamoja na wanaoshuka chini kwa wafu.


Wamisri wataangamia pamoja na watu waliouawa katika vita. Upanga uko tayari kuangamiza Misri pamoja na watu wake wengi.


Hawakuzikwa pamoja na mashujaa wa zamani, ambao walikwenda katika kuzimu kwa wafu wakiwa na silaha zao, mapanga yao chini ya vichwa vyao na ngao zao juu ya miili yao. Mashujaa hao walipokuwa wangali wanaishi walijaza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima.


Hata ukiruka juu kama tai, ukifanya makao yako kati ya nyota, mimi nitakushusha chini tu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


Nawe, muji Kapernaumu, unafikiri kwamba utapandishwa mpaka juu mbinguni? Utashushwa mpaka chini katika kuzimu. Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yako ingalifanyika katika Sodoma, muji ule ungekuwa ungali hata leo.


Yeye akatoka Nazareti, akaenda kukaa Kapernaumu, pembeni ya ziwa la Galilaya, katika wilaya ya Zebuluni na ya Nafutali, kusudi yatimie


Na kule mutalia na kusaga meno, mutakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika Ufalme wa Mungu. Lakini ninyi mutakuwa mumetupwa inje!


Alipokuwa katika jehenamu akiteswa sana, akainua macho, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro akiwa pembeni yake.


Kwa nini tuende huko wakati tumevunjika moyo kwa hofu? Wametuambia kwamba watu wa huko ni wakubwa na warefu kuliko sisi, na kwamba miji yao ni mikubwa na yenye kuta zinazofika katika mawingu. Tena wamesema kwamba waliwaona wale wazao wa Anaki!’


Kwa maana Mungu hakuwahurumia wale wamalaika waliofanya zambi, lakini aliwatupa katika jehenamu. Wao wanalindwa mule wakifungwa minyororo katika giza nzito wakingojea Siku ile ya hukumu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ