Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 1:76 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

76 Na wewe, mutoto wangu, utaitwa nabii wa Mungu Mukubwa, maana utatangulia mbele ya kufika kwa Bwana, kusudi umutengenezee njia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 1:76
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini juu ya Sayuni itasemwa: “Sayuni ni mama yao wote; Mungu Mukubwa atauimarisha.”


Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.


Herode alitaka kumwua Yoane, lakini aliwaogopa watu kwa maana wote walimuhesabia Yoane kuwa nabii.


Lakini vilevile kwa kuwa tunaogopa watu hawa, hatuwezi kusema kwamba yalitoka kwa mutu; kwa maana watu hawa wote wanasadiki kwamba Yoane alikuwa nabii.”


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Yoane ndiye yule Mungu aliyemutaja kwa njia ya nabii Isaya akisema: “Sauti inatangaza katika jangwa: ‘Mutengeneze njia ya Bwana, munyooshe pahali atakapopita!’ ”


Vilevile hatuwezi kusema kama yalitoka kwa watu…” (Waliogopa kundi la watu kwa maana wote walisadiki kama Yoane alikuwa nabii wa kweli).


Yeye atakuwa mwenye mamlaka, na ataitwa Mwana wa Mungu Mukubwa. Bwana Mungu atamuweka kuwa mutawala wa ufalme wa babu yake Daudi.


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Lakini muwapende waadui zenu, muwatendee mema na muwakopeshe pasipo kutumainia kurudishiwa kitu. Halafu mutapewa zawadi kubwa na mutakuwa kweli watoto wa Mungu Mukubwa kwa sababu yeye ni mwema kwa watu waovu wasiokuwa na shukrani.


Yoane akajibu: “Mimi ni sauti inayotangaza katika jangwa: ‘Munyooshe njia ya Bwana,’ ” sawa vile nabii Isaya alivyosema.


anayekuja nyuma yangu. Mimi sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”


Ninyi wenyewe ni washuhuda wangu kwamba nilisema: ‘Mimi si Kristo, lakini nimetumwa mbele yake.’


Mwanamuke yule akaendelea kumufuata Paulo na sisi, akilalamika akisema: “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Mukubwa. Wanawatangazia ninyi namna gani munavyoweza kuokolewa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ