Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 1:68 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

68 “Asifiwe Bwana, Mungu wa Waisraeli, maana amewasaidia watu wake na kuwakomboa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 1:68
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atukuzwe Mungu Mukubwa, aliyetia waadui zako katika mikono yako!” Naye Abramu akamupa Melkisedeki sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo.


akisema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hajasahau wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Yawe ameniongoza mimi mwenyewe moja kwa moja mpaka kwa jamaa ya bwana wangu!”


Tena akasema: “Semu abarikiwe na Yawe, Mungu wangu! Kanana akuwe mutumwa wake.


na kuomba akisema: ‘Asifiwe Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye amemufanya muzao wangu kuwa mufalme kwa pahali pangu, na ambaye amenipa maisha hata nimeyaona mambo hayo.’ ”


akasema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, maana kwa nguvu yake ametimiza ahadi yake aliyomupa baba yangu Daudi, akisema:


Halafu Daudi akamutukuza Yawe mbele ya mukutano wote, akisema: “Utukuzwe milele na milele, ee Yawe, Mungu wa baba yetu Israeli.


Kisha, mufalme Daudi akawaambia wote waliokusanyika: “Mumusifu Yawe, Mungu wenu.” Na wote waliokusanyika wakamutukuza Yawe, Mungu wa babu zao, wakainama mbele yake na kumwabudu Yawe na kumutolea mufalme Daudi heshima.


Yawe, Mungu wa Israeli, asifiwe tangu milele na hata milele! Na watu wote waseme: “Amina!” Haleluia!


Aliwakomboa watu wake na kufanya nao agano la milele. Yeye ni mutakatifu na wa kutisha sana!


Yeye atawakomboa watu wa Israeli kutoka katika maovu yao yote.


Wewe unaniimarisha katika ukamilifu; utanichunga mbele yako milele.


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Aliahidi kutuokoa toka mikono ya waadui zetu, ndio wale wanaotuchukia.


Watakuharibu kabisa pamoja na wakaaji wako. Hawatakuachia hata jengo moja lisilobomolewa kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuja kukuokoa.”


Basi, akafika saa ile ile, akaanza kumushukuru Mungu. Naye akaeleza habari za mutoto huyo kwa watu wote waliokuwa wakingojea jinsi Mungu atakavyokomboa Yerusalema.


Sisi tulikuwa na tumaini kwamba yeye ndiye atakayekomboa Waisraeli. Lakini sasa, leo ni siku ya tatu tangu mambo hayo yalipofanyika.


Watu wote wakashikwa na woga, nao wakamutukuza Mungu, wakisema: “Nabii mukubwa ametokea tena kwetu! Mungu amekuja kuwasaidia watu wake.”


Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.


Kwa njia ya damu ya Kristo, sisi tumekombolewa, maana yake zambi zetu zimesamehewa. Hivi Mungu ameonyesha uwingi wa neema yake


Aliingia mara moja tu katika Pahali Patakatifu Sana. Naye hakupeleka mule sadaka ya damu ya mbuzi na ya ngombe, lakini alipeleka damu yake mwenyewe. Na kwa njia ile akatukomboa kwa milele.


Tumusifu Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kubwa ametupatia uzima mupya kwa njia ya kumufufua Yesu Kristo. Na kwa hiyo tumepata tumaini lenye uzima,


Daudi akamwambia Abigaili: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, aliyekutuma leo kukutana nami.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ