Imani yenu na upendo wenu vinakuwa na musingi katika tumaini mulilowekewa mbinguni. Mulisikia juu ya tumaini lile mara ya kwanza wakati mulipohubiriwa ujumbe wa ukweli ni kusema Habari Njema.
Kijana mumoja kati ya watumishi akasema: “Nimemwona kijana mumoja wa Yese, wa muji wa Betelehemu. Kijana yule ana ujuzi wa kupiga kinubi. Yule kijana ni shujaa, hodari wa kupigana katika vita, ana hekima katika kusema na mwenye umbo zuri; Yawe yuko pamoja naye.”