Basi wandugu zangu, mukumbuke vile mulivyoitwa na Mungu, kwamba si wengi kati yenu wenye hekima kufuatana na mafikiri ya watu; si wengi kati yenu wanaokuwa wenye nguvu, wala wenye vyeo.
Sasa mumekwisha kupata vyote munavyohitaji! Mumekwisha kuwa watajiri! Munakuwa wafalme ingawa sisi hatuko wafalme. Heri mungekuwa kweli watawala kusudi nasi vilevile tupate kutawala pamoja nanyi.
Wale ambao zamani walikuwa na chakula tele, sasa wanafanya kazi wapate chakula. Lakini waliokuwa na njaa, sasa hawana njaa tena. Mwanamuke tasa, amezaa watoto saba. Lakini mama mwenye watoto wengi, sasa ameachwa bila mutoto.