50 Yeye anawasikilia wale wanaomwogopa huruma kwa vizazi vyote.
“Nitasimamisha agano langu nawe, wazao wako na vizazi vyao vyote milele; nitakuwa Mungu wako na Mungu wa wazao wako milele.
mutaniabudu mimi Yawe, Mungu wenu, nami nitawaokoa kutoka katika mikono ya waadui zenu.”
Kama vile anga linavyokuwa juu mbali na dunia, ndivyo kipimo cha wema wake kinavyokuwa kwa watu wanaomwabudu.
atawabariki wote wanaomwabudu, atawabariki wakubwa kama vile wadogo.
Wote wanaomwabudu Yawe waseme: “Wema wake unadumu milele.”
Anajibia mahitaji yao wote wanaomwabudu; anasikia kilio chao na kuwaokoa.
lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.
Funga midomo ya hao watu waongo, watu wenye kiburi na majivuno, ambao wanazarau watu wa haki.
Ninasikiliza yale Yawe anayosema, maana anaahidi kuwapa watu wake amani, watu wake mwenyewe wasiporudilia upumbafu wao.
Lakini ninawatendea mema maelfu ya wale wanaonipenda na kushika amri zangu.
sababu Mungu Mwenye Uwezo, amenitendea maajabu. Jina lake ni takatifu.
Kisha sauti ikasikilika toka kwenye kiti cha kifalme ikasema: “Mumusifu Mungu wetu ninyi watumishi wake wote, ninyi wote munaomuheshimu, wakubwa na wadogo!”