Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 1:48 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

48 kwa maana ameniangalia kwa huruma, mimi mujakazi wake munyenyekevu. Tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 1:48
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lea akasema: “Bahati njema! Sasa wanawake wataniita heri.” Kwa hiyo akamwita mutoto yule Aseri.


Kwa hiyo basi, umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Nilikutoa katika shamba la malisho ya nyama ulimokuwa unawachunga kondoo, kusudi ukuwe mukubwa wa watu wangu Waisraeli.


Yawe atajenga upya Sayuni, na kuonyesha utukufu wake.


Alitukumbuka wakati wa uzaifu wetu. Wema wake unadumu milele.


Ee Yawe, ingawa wewe uko juu ya wote, unawaangalia wanyenyekevu kwa wema; lakini, unatambua wenye kiburi kwa mbali.


Jina la mufalme litukuzwe siku zote; utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa. Kwake mataifa yote yabarikiwe; watu wote wamwite mwenye heri!


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Halafu mataifa yote yatawaita ninyi watu waliobarikiwa, maana inchi yenu itakuwa inchi ya furaha. –Ni Yawe, Mungu Mukubwa anayesema hivyo.


Malaika akamufikia kwenye nyumba yao na kumwambia: “Salamu kwako, wewe uliyejaliwa neema kutoka kwa Mungu! Bwana yuko pamoja nawe.”


akasema kwa sauti kubwa: “Wewe umebarikiwa kuliko wanawake wote, na mutoto utakayemuzaa amebarikiwa!


Heri kwako wewe uliyesadiki kwamba maneno yale uliyoambiwa kutoka kwa Bwana yatatimizwa!”


sababu Mungu Mwenye Uwezo, amenitendea maajabu. Jina lake ni takatifu.


Yesu alipokuwa akisema maneno hayo, mwanamuke mumoja kati ya kundi la watu akasema kwa sauti kubwa: “Heri mwanamuke yule aliyekuzaa na kukunyonyesha!”


Akafanya kiapo akisema: “Ee Yawe wa majeshi, kama tu utayaangalia mateso yangu mimi mujakazi wako, ukinikumbuka mimi, bila kunisahau, mimi mujakazi wako, ukinijalia mimi mujakazi wako mutoto mwanaume, nitakupa wewe Yawe mutoto huyo akuwe wako maisha yake yote; wembe hautapita kwenye kichwa chake hata kidogo.”


Anawainua wazaifu toka katika mavumbi, anawanyanyua wakosefu toka katika majivu, na kuwaikalisha pamoja na wakubwa, na kuwarizisha viti vya heshima. Maana, minara ya dunia ni ya Yawe; yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ