Mimba hiyo ilikuwa ya mapacha. Watoto hao waligongana ndani ya tumbo la Rebeka, naye akasema: “Kama hivi ndivyo mambo yanavyokuwa, kwa nini kuishi?” Basi, akakwenda kumwuliza Yawe.
Lakini Stefano akijazwa na Roho Mutakatifu, akakaza macho kuelekea mbingu akaona mwangaza wa utukufu wa Mungu naye Yesu akisimama na mamlaka karibu na Mungu.
Basi Anania akaenda. Alipofika ndani ya nyumba ambamo Saulo alikuwa, akaweka mikono juu yake na kumwambia: “Ndugu Saulo, Bwana Yesu aliyekutokea katika njia ulipokuwa ukikuja huku, amenituma kusudi upate kuona tena na kujazwa na Roho Mutakatifu.”