Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 1:36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

36 Hata Elizabeti wa jamaa yako, amepata mimba, naye atazaa mutoto mwanaume, ijapokuwa yeye ni muzee. Yeye aliyekuwa akiitwa tasa, sasa huu ni mwezi wa sita wa mimba yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 1:36
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sarai hakukuwa na mutoto kwa sababu alikuwa tasa.


Basi, Sarai, muke wa Abramu, alikuwa bado hajamuzalia mutoto, naye alikuwa na mujakazi aliyeitwa Hagari, kutoka Misri.


Abrahamu na Sara walikuwa wazee sana, naye Sara hangeweza tena kuzaa.


Basi, Abrahamu akiwa muzee, Sara akapata mimba, akamuzalia mutoto mwanaume, wakati uleule Mungu aliotaja.


Lakini yule mwanamuke akapata mimba na kuzaa mutoto wakati kama ule mwaka uliofuata, kama vile Elisha alivyokuwa amemwambia.


wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa,


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Kwa maana hakuna kisichowezekana kwa Mungu.”


Katika siku Herode alipokuwa mufalme wa Yudea, kulikuwa kuhani mumoja, aliyeitwa Zakaria, wa kundi la makuhani wa ukoo wa Abiya. Muke wake Elizabeti alikuwa vilevile wa uzao wa Kuhani Mukubwa Haruni.


Kwa njia ya imani, Sara mwenyewe vilevile, ijapokuwa alikuwa muzee sana, alijaliwa uwezo wa kupata mimba kwa sababu aliamini kwamba Mungu atatimiza ahadi yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ