Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 1:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 1:35
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nani anayeweza kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu? Hakuna anayeweza.


kefu sasa mwanadamu anayekuwa chukizo na mupotovu, mwanadamu anayetenda uovu kama kunywa maji!


Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?


Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Ninaitikia kabisa makosa yangu, siku zote ninaona waziwazi zambi yangu.


Hii ndiyo habari ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Maria, mama yake, alikuwa muchumba wa Yosefu. Lakini mbele hawajakaa pamoja, akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mutakatifu.


Naye alipokuwa angali akifikiri juu ya maneno hayo, malaika wa Bwana akamutokea katika ndoto na kumwambia hivi: “Wewe Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumwoa muchumba wako Maria, kwa maana mimba yake imetokana na uwezo wa Roho Mutakatifu.


Basi wanafunzi waliokuwa ndani ya chombo wakapiga magoti mbele ya Yesu, wakisema: “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu!”


Mukubwa wa waaskari na wale waliokuwa pamoja naye wakimuchunga Yesu walipoona tetemeko la inchi na mambo yote yaliyofanyika, wakaogopa sana, na kusema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”


Shetani akamufikia na kumwambia: “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yageuke kuwa mikate.”


Huu ndio mwanzo wa Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.


“Kuna maneno gani kati yako na sisi, wewe Yesu wa Nazareti? Ulikuja kutuangamiza? Ninakutambua wewe ni nani: wewe ni Mutakatifu aliyetumwa na Mungu.”


Alimutuma kwa binti mumoja aliyekuwa muchumba wa mutu mumoja wa ukoo wa mufalme Daudi, aliyeitwa Yosefu. Jina la yule binti liliitwa Maria.


Maria akamwuliza malaika: “Jambo hili litawezekana namna gani kwa maana mimi ningali bikira?”


Hata Elizabeti wa jamaa yako, amepata mimba, naye atazaa mutoto mwanaume, ijapokuwa yeye ni muzee. Yeye aliyekuwa akiitwa tasa, sasa huu ni mwezi wa sita wa mimba yake.


Mimi nimeona mambo haya, nami ninashuhudia kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu.”


Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”


Lakini hii imeandikwa kusudi mupate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mupate uzima katika jina lake.


Walipokuwa wakiendelea na safari, wakafika kwenye nafasi moja kwenye maji, yule mukubwa akasema: “Hapa kuna maji. Ni kitu gani kinachonizuiza nisibatizwe?” [


Na sasa si mimi ninayekuwa ningali nikiishi, lakini ni Kristo anayeishi ndani yangu. Maisha ninayoishi sasa, inatokana na kumwamini Mwana wa Mungu aliyenipenda na kutoa maisha yake kwa ajili yangu.


Zamani, sisi wote vilevile tulikuwa kama wao. Tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kimwili na kutenda kufuatana na mapenzi ya mwili na roho zetu. Kwa sababu ya hali yetu ya kimwili, hatungeponyoka kasirani ya Mungu kama wengine.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ