Petro alipokuwa angali na wasiwasi, naye akijiuliza juu ya maana ya maono yale, wale watu waliotumwa na Kornelio wakafika mbele ya mulango kwa maana walikuwa wamekwisha kujulishwa nafasi gani kunapokuwa nyumba ya Simoni.
Kornelio akamukazia macho akiwa ameshikwa na woga, akamwuliza: “Bwana, ni nini?” Malaika akamujibu: “Mungu amesikia maombi yako na kupendezwa na misaada unayotoa kwa wamasikini, na kwa hiyo anakukumbuka.