27 Alimutuma kwa binti mumoja aliyekuwa muchumba wa mutu mumoja wa ukoo wa mufalme Daudi, aliyeitwa Yosefu. Jina la yule binti liliitwa Maria.
Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”
Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.
Utasitasita mpaka wakati gani, ewe binti usiyekuwa mwaminifu? Maana, mimi nimefanya kitu kipya katika dunia; mwanamuke anamulinda mwanaume.
Hii ndiyo habari ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Maria, mama yake, alikuwa muchumba wa Yosefu. Lakini mbele hawajakaa pamoja, akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mutakatifu.
“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).
Malaika akamufikia kwenye nyumba yao na kumwambia: “Salamu kwako, wewe uliyejaliwa neema kutoka kwa Mungu! Bwana yuko pamoja nawe.”