Luka 1:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
22 Alipotoka inje, hakuweza kusema nao, na watu wakatambua kwamba amepata maono ndani ya hekalu. Lakini alikuwa akifanya alama kwa mikono, kwa sababu alibaki bubu.
Naye akawanyamazisha kwa kunyoosha mukono, kuwaelezea namna Bwana alivyomwondoa katika kifungo. Akawaambia tena: “Muwaelezee Yakobo na wandugu wengine waamini habari hizi.” Kisha Petro akaondoka na kwenda nafasi ingine.
Watu wamoja katika mukutano wakaeleza mambo yaliyotokea kwa Alesanduro, yeye aliyesukumwa na Wayuda kwenda kusema mbele ya watu. Basi Alesanduro akainua mukono kwa kuwanyamazisha watu, kwa maana alitaka kujitetea mbele yao.
Yule mukubwa wa kundi la waaskari akamuruhusu. Basi Paulo akasimama juu ya ngazi, akainua mukono kwa kuwaalika watu wanyamaze. Na watu waliponyamaza kabisa, Paulo akawaambia maneno haya katika luga ya Kiebrania: