Luka 1:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
20 Maneno yale yatatimia kwa wakati wake uliopangwa, lakini kwa sababu haukuyasadiki, utakuwa bubu. Hautaweza kusema mpaka siku ile mambo hayo yatakapotimia.”
Yule jemedari mulinzi wa mufalme alikuwa amemwambia Elisha: “Hata kama Yawe mwenyewe angefanya madirisha mbinguni, jambo hilo litawezekana?” Naye Elisha alikuwa amemujibu: “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hautakula.”
Lakini Yawe akamwambia Musa na Haruni: Kwa sababu ninyi hamukuniamini mimi, wala kuniheshimu mbele ya macho ya Waisraeli, basi kwa sababu hiyo hamutaingiza watu hawa katika ile inchi niliyowapa.
Kwa mwisho Yesu akawatokea wanafunzi kumi na mumoja walipokuwa wakikula. Naye akawakaripia kwa sababu ya kutokuamini kwao na kwa sababu ya ugumu wao. Kwa maana hawakusadikia wale waliomwona nyuma ya kufufuka kwake.
Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”
Alipotoka inje, hakuweza kusema nao, na watu wakatambua kwamba amepata maono ndani ya hekalu. Lakini alikuwa akifanya alama kwa mikono, kwa sababu alibaki bubu.
Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.