Luka 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
13 Lakini yule malaika akamwambia: “Zakaria, usiogope, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Muke wako Elizabeti atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yoane.
Mungu akamujibu: “Hapana. Muke wako Sara atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita Isaka. Nitaimarisha agano langu kwake na wazao wake, kuwa agano la milele.
Nikalala na muke wangu ambaye vilevile ni nabii, akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Yawe akaniambia: Umupe mutoto huyo jina “Teka-haraka-nyanganya-upesi.”
Kwa hiyo yeye akaniambia: Danieli, usiogope. Mungu alisikia maombi yako tangu siku ile ya kwanza ulipoamua kujinyenyekeza mbele yake kusudi upate ufahamu. Mimi nimekuja kwa ajili ya maombi yako hayo.
Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Yezereheli”, maana kisha siku chache tu, nitaiazibu jamaa ya Yehu kwa mauaji aliyofanya katika bonde la Yezereheli. Hivi nitavunja ufalme katika taifa la Israeli.
Lakini kijana yule akawaambia: “Musishituke! Munamutafuta Yesu wa Nazareti aliyetundikwa juu ya musalaba. Yeye amefufuka, hayuko hapa. Muangalie, hapa ni pahali walipomuweka.
Ilipotimia siku ya kumutahiri mutoto, ndiyo siku ya nane tangu alipozaliwa, wakamupa jina lake Yesu. Jina hili ni lile malaika alilojulisha mbele mama yake hajabeba mimba.