11 Halafu malaika wa Bwana akamutokea Zakaria, akisimama upande wa kuume wa mazabahu ya kuchomea ubani.
Kusudi asikufe, ataleta ubani ule mbele ya Yawe na kuutia katika moto kusudi moshi wa ubani ule ufunike kifuniko cha Sanduku la Agano.
Malaika akamujibu: “Mimi ni Gabrieli, anayebaki karibu na Mungu! Nimetumwa kusema nawe, kwa kukuletea habari hii njema.
Malaika akamufikia kwenye nyumba yao na kumwambia: “Salamu kwako, wewe uliyejaliwa neema kutoka kwa Mungu! Bwana yuko pamoja nawe.”
Lakini malaika akawaambia: “Musiogope, kwa sababu ninawaletea Habari Njema itakayofurahisha sana watu wote.
Na kwa rafla malaika wa Bwana akawatokea, na mwangaza wa utukufu wa Bwana ukawazunguka. Nao wakaogopa sana.
Lakini usiku malaika wa Bwana akafungua milango ya kifungo, akawaondosha mitume mule na kuwaambia:
Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.
Malaika wa sita akapiga baragumu. Halafu nikasikia sauti moja ikitokea kwenye pembe ine za mazabahu ya zahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.
Siku moja, malaika wa Yawe akamutokea yule mwanamuke, akamwambia: “Wewe ni tasa, hauna watoto. Lakini utapata mimba na kumuzaa mutoto mwanaume.
Yawe akalisikia ombi la Manoa, na yule malaika wa Mungu akamwendea tena yule mwanamuke alipokuwa akiikaa katika shamba. Lakini mume wake Manoa hakukuwa pamoja naye.