Mufalme wa Misri akauliza habari juu ya nyama wa Waisraeli. Wakamwambia kwamba hakuna nyama wao hata mumoja aliyekufa. Hata hivyo, Mufalme akabaki akifanya moyo wake kuwa mugumu, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.
Majivu hayo yatakuwa vumbi nyembamba itakayoenea juu ya inchi yote ya Misri. Yatasababisha majipu yatakayopasuka na kuwa vidonda kwa watu na nyama kila pahali katika inchi ya Misri.”