Katikati ya usiku, Yawe akawaua wazaliwa wa kwanza wote wa Misri. Wote walikufa, tangu muzaliwa wa kwanza wa mufalme wa Misri, murizi wa ufalme, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mufungwa katika kifungo. Hata wazaliwa wa kwanza wa nyama nao walikufa.
Lakini Musa akamujibu: “Hapana! Haifai kufanya hivyo, maana sadaka tutakazomutolea Yawe, Mungu wetu, zitawachukiza Wamisri. Wamisri wakituona tunatoa sadaka ambazo ni chukizo kwao, si watatupiga mawe?
Mvua hiyo ya mawe ilivunjavunja kila kitu katika mashamba na kila pahali katika inchi ya Misri, nyama na watu. Mawe ya mvua yakavunjavunja mimea yote na miti katika mashamba.