Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 9:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Lakini mufalme wa Misri alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo vimekoma, akarudilia zambi yake tena. Akafanya moyo wake kuwa mugumu, yeye pamoja na wakubwa wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 9:34
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati alipokuwa katika taabu zaidi, mufalme huyu Ahazi alizidi kumwasi Yawe.


Naye hakujinyenyekeza mbele za Yawe, kama vile Manase alivyofanya, lakini yeye aliongeza kutenda makosa zaidi.


Sedekia alimwasi vilevile mufalme Nebukadneza aliyekuwa amemufanya aape kwa jina la Mungu kwamba hatamwasi. Alikuwa mupotovu sana na kufanya moyo mugumu, akakataa kumugeukia Yawe, Mungu wa Israeli.


Yawe akamwambia Musa: “Utakapofika Misri, uhakikishe kwamba umetenda mbele ya mufalme wa Misri miujiza yote niliyokupa uwezo wa kuifanya. Lakini mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye hatawaachilia Waisraeli waondoke.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Moyo wa mufalme wa Misri umekuwa mugumu. Anakataa kuwaacha Waisraeli waondoke.


Wale wachawi wakamwambia mufalme wa Misri: “Hii ni kazi ya mukono wa Mungu.” Lakini moyo wa mufalme ukaendelea kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Basi, Musa akaondoka katika nyumba ya mufalme, akatoka inje ya muji. Kisha akainua mikono yake kumwomba Yawe. Ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua ikaacha kunyesha katika dunia.


Basi, kama vile Yawe alivyomwambia Musa, moyo wa mufalme wa Misri ulikuwa mugumu, yeye na wakubwa wake, akakataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke.


Kwa vile uovu hauazibiwi haraka, mioyo ya wanadamu inakusudia kutenda mabaya.


Kwa nini munafanya mioyo yenu kuwa migumu kama Wamisri na Mufalme wao? Mungu alipowachekelea Wamisri, hawakuwaacha Waisraeli waondoke, nao wakaondoka?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ