Yawe akamwambia Musa: “Utakapofika Misri, uhakikishe kwamba umetenda mbele ya mufalme wa Misri miujiza yote niliyokupa uwezo wa kuifanya. Lakini mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye hatawaachilia Waisraeli waondoke.
Mufalme wa Misri hatakusikiliza. Na hapo nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuazibu vikali inchi ya Misri na kuwatoa watu wangu, makabila ya Israeli, kutoka Misri. Nitafanya hivyo kwa matendo makubwa ya hukumu juu ya Misri,
Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa mufalme wa Misri. Mimi nimefanya moyo wake kuwa mugumu na wa wakubwa wake kusudi nipate kuonyesha vitambulisho hivi kati yao,
Basi, Musa na Haruni walifanya maajabu hayo yote mbele ya mufalme wa Misri. Lakini Yawe alifanya moyo wa mufalme kuwa mugumu, akakataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke katika inchi yake.
Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.
Mufalme wa Misri akauliza habari juu ya nyama wa Waisraeli. Wakamwambia kwamba hakuna nyama wao hata mumoja aliyekufa. Hata hivyo, Mufalme akabaki akifanya moyo wake kuwa mugumu, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.