Basi, mufalme Yeroboamu akamwambia nabii: “Tafazali, umusihi Yawe, Mungu wako, uniombee mukono wangu upate kupona.” Naye nabii akamwomba Yawe, na mukono wa mufalme ukapona, ukarudia kwa hali yake ya zamani.
Mufalme wa Misri aliposikia kwamba Waisraeli wamekimbia, yeye na wakubwa wake walibadilisha mafikiri yao, wakasema: “Tumefanya nini kwa kuwaachilia Waisraeli waende zao wasitutumikie tena?”
Lakini Musa akamusihi Yawe, Mungu wake, akisema: Ee Yawe, kwa nini hasira yako inawaka vikali juu ya watu wako uliowatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo mukubwa na mukono wenye nguvu?
Wale wachawi wakamwambia mufalme wa Misri: “Hii ni kazi ya mukono wa Mungu.” Lakini moyo wa mufalme ukaendelea kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.
Basi, Musa akaondoka katika nyumba ya mufalme, akatoka inje ya muji. Kisha akainua mikono yake kumwomba Yawe. Ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua ikaacha kunyesha katika dunia.
Basi, watu wakamwendea Musa, wakamwambia: Tumetenda zambi kwa kumunungunikia Yawe na wewe vilevile. Umwombe Yawe atuondolee nyoka hawa. Kwa hiyo, Musa akawaombea watu.
Hivyo wakamwambia Samweli: “Tafazali, utuombee sisi watumishi wako kwa Yawe, Mungu wako, kusudi tusikufe; kwa sababu tumezidisha zambi zetu kwa uovu huo wa kujitakia mufalme.”