Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 8:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mufalme wa Misri akamwambia: “Kesho.” Musa akasema: “Nitafanya kama vile unavyosema, kusudi ujue kwamba hakuna yeyote anayelingana na Yawe, Mungu wetu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 8:6
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kutokana na yale tuliyosikia, wewe Yawe ni mukubwa. Hakuna anayekuwa kama wewe, na hakuna Mungu mwingine lakini wewe.


Aliomba akisema: “Ee, Yawe, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu mwingine kama wewe, mbinguni au katika dunia. Wewe ni mwaminifu, maana umetimiza agano lako na kutenda mema kwa watumishi wako wanaoishi wakikutii kwa moyo wao wote.


Vyura wakajaa juu ya inchi yao, hata katika nyumba ya mufalme.


Aliwapelekea makundi ya mainzi yaliyowasumbua, na vyura waliowaletea hasara.


Ee Bwana, hakuna mungu mwingine anayekuwa kama wewe; hakuna anayeweza kufanya unayofanya wewe.


Mbele milima haijakuwa, mbele haujauumba ulimwengu, wewe ndiwe Mungu, milele na milele.


na ninyi mupate kuwaelezea watoto wenu na wajukuu wenu jinsi nilivyowachekelea Wamisri kwa kuonyesha vitambulisho vile kati yao. Hivyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.”


“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?


Yawe akamwambia Musa: “Umwambie Haruni atwae fimbo yake na kuiinua juu ya maji ya Misri, juu ya mito yote, mifereji, visima na maji yao yote, nayo yatakuwa damu. Kutakuwa damu katika inchi yote, na hata katika vyombo vyote vya muti na vya mawe.”


Maana mara hii, wewe mwenyewe, wakubwa wako na watu wako mutapatwa na mapigo yangu makali. Nawe utatambua kwamba hakuna yeyote katika dunia anayekuwa kama mimi.


Musa akamwambia: “Mara tu nitakapotoka inje ya muji nitainua mikono na kumwomba Yawe. Ngurumo itakoma na hakutakuwa mvua ya mawe tena kusudi utambue kwamba dunia ni ya Yawe.


Ninyi Waisraeli ni washuhuda wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwachagua mukuwe watumishi wangu, mupate kunijua na kuniamini, kwamba mimi ni Mungu. Mbele yangu hakukuwa mungu mwingine, wala hakutakuwa mungu mwingine nyuma yangu.


Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba ni kichafu kwenu.


Hata waadui zetu wenyewe wanajua wazi, mulinzi wao hana nguvu kama mulinzi wetu.


Musa akamalizia kwa kusema: “Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako, yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia, anapita juu katika anga katika utukufu wake.


Ninyi mulijaliwa kuona mambo hayo, kusudi mupate kutambua kwamba Yawe ndiye peke yake Mungu na wala hakuna mwingine.


Halafu nikaona pepo wachafu watatu wanaofanana na vyura wakitoka ndani ya kinywa cha yule nyoka mukubwa, na ndani ya kinywa cha yule nyama wa ajabu na cha yule nabii wa uongo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ