Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 8:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kisha mufalme wa Misri akamwita Musa na Haruni, akawaambia: “Musihi Yawe, kusudi aniondolee mimi na watu wangu vyura hawa, nami nitawaacha Waisraeli wajiendee na kutoa sadaka kwa Yawe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 8:4
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, mufalme Yeroboamu akamwambia nabii: “Tafazali, umusihi Yawe, Mungu wako, uniombee mukono wangu upate kupona.” Naye nabii akamwomba Yawe, na mukono wa mufalme ukapona, ukarudia kwa hali yake ya zamani.


aliwazarau wakubwa waliowatesa, akawazungusha katika jangwa lisilokuwa na njia.


Kwa hiyo sasa ninawasihi munisamehe zambi yangu mara hii, muniombee kwa Yawe, Mungu wenu, aniondolee kifo hiki.”


Basi, mufalme wa Misri akasema: “Nitawaacha mujiendee kutoa sadaka kwa Yawe, Mungu wenu, katika jangwa. Lakini musiende mbali sana. Muniombee mimi.”


Lakini wachawi wa Misri kwa uchawi wao vilevile wakaleta vyura katika inchi ya Misri.


Musa akamujibu mufalme wa Misri: “Basi! Unaweza kutaja wakati unaotaka nikuombee kwa Mungu, niwaombee wakubwa wako na watu wako. Nitamwomba awaangamize vyura hawa wanaokuwa katika nyumba zenu. Watabaki tu katika muto Nili!”


Mumwombe Yawe maana ngurumo hii na mvua ya mawe vimezidi. Mimi nitawaacha muondoke na wala hamutabakia tena.”


Wakubwa wa muji wa Soani ni wapumbafu kabisa, washauri wa Mufalme wa Misri wanatoa shauri la kijinga! Kila mumoja anaweza namna gani kumwambia Mufalme wa Misri: Mimi ni wa uzao wa wenye hekima, wa uzao wa wafalme wa zamani!


Yawe atawaazibu Wamisri na kuwaponya. Nao watamurudilia, naye atayasikiliza maombi yao na kuwaponya.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Basi, watu wakamwendea Musa, wakamwambia: Tumetenda zambi kwa kumunungunikia Yawe na wewe vilevile. Umwombe Yawe atuondolee nyoka hawa. Kwa hiyo, Musa akawaombea watu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ