Lakini Yoseba, binti ya mufalme Yoramu alimutwaa Yoasi, akamuchukua kwa siri kutoka kati ya wana wa mufalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamuficha yeye pamoja na yaya wake, katika chumba cha kulala. Hivyo Yoseba, binti ya mufalme Yoramu, muke wa kuhani Yoyada, kwa sababu alikuwa dada ya Ahazia, akamuficha Yoasi kusudi Atalia asimwone na kumwua.