Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 8:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kisha Yawe akamwambia Musa: “Kesho amuka asubui mapema umwendee mufalme wa Misri wakati anapokwenda kwenye muto umwambie: ‘Yawe anasema hivi: Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 8:16
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akaamuru, kukatokea makundi ya mainzi, na imbu katika inchi yote.


Nami ninakuambia: Umwache mwana wangu aondoke, kusudi anitumikie! Kama ukikataa kumwachilia aondoke, angalia nitamwua muzaliwa wako wa kwanza mwanaume.’ ”


Kisha, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri, wakamwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke, wanifanyie sikukuu katika jangwa.’ ”


Wale wachawi wakamwambia mufalme wa Misri: “Hii ni kazi ya mukono wa Mungu.” Lakini moyo wa mufalme ukaendelea kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Kama ukikataa kuwaacha waondoke, basi, nitakuletea makundi ya mainzi, wewe, wakubwa wako na watu wako wote. Wataingia kwenye nyumba zenu na nyumba zote za Wamisri zitajaa makundi ya mainzi na inchi yote ya Misri vilevile.


Lakini siku hiyo sehemu ya Goseni watu wangu wanakoishi nitaikinga. Kule mainzi wale hawatakuwa. Kwa hiyo utatambua kwamba mimi Yawe ninatenda mambo katika inchi yako.


Musa akamujibu mufalme wa Misri: “Basi! Unaweza kutaja wakati unaotaka nikuombee kwa Mungu, niwaombee wakubwa wako na watu wako. Nitamwomba awaangamize vyura hawa wanaokuwa katika nyumba zenu. Watabaki tu katika muto Nili!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ