Lakini Musa akamusihi Yawe, Mungu wake, akisema: Ee Yawe, kwa nini hasira yako inawaka vikali juu ya watu wako uliowatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo mukubwa na mukono wenye nguvu?
Musa na Haruni wakafanya hivyo. Haruni akainua fimbo yake na kupiga mavumbi, nayo yakageuka kuwa chawa nao wakakuwa juu ya watu na nyama. Mavumbi yote katika inchi yote ya Misri yakageuka kuwa chawa.
Basi, Musa akaondoka katika nyumba ya mufalme, akatoka inje ya muji. Kisha akainua mikono yake kumwomba Yawe. Ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua ikaacha kunyesha katika dunia.