Kutoka 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 Lakini mufalme wa Misri alipoona kwamba inchi imepata utulivu, akakuwa na moyo mugumu tena, wala hakusikiliza Musa na Haruni, kama vile Yawe alivyokuwa amesema.
Yawe akamwambia Musa: “Utakapofika Misri, uhakikishe kwamba umetenda mbele ya mufalme wa Misri miujiza yote niliyokupa uwezo wa kuifanya. Lakini mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye hatawaachilia Waisraeli waondoke.
Musa na Haruni wakafanya hivyo. Haruni akainua fimbo yake na kupiga mavumbi, nayo yakageuka kuwa chawa nao wakakuwa juu ya watu na nyama. Mavumbi yote katika inchi yote ya Misri yakageuka kuwa chawa.