Basi, Musa akainua fimbo yake juu ya inchi ya Misri. Yawe akaleta upepo toka upande wa mashariki, ukavuma juu ya inchi muchana kutwa na usiku kucha. Kulipokucha, ule upepo ukaleta nzige.
Basi, Musa akatwaa muke wake na watoto wake, akawapandisha juu ya punda, akaanza safari ya kurudi Misri. Katika mukono wake alishika ile fimbo aliyoamuriwa na Mungu aitwae.
Basi, Musa akainua fimbo yake kuelekea mbinguni. Naye Yawe akaleta mvua ya mawe na ngurumo, umeme ukapiga inchi. Yawe alinyesha mvua ya mawe juu ya inchi ya Misri,
Umwambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana na wewe mufalme wa Misri, wewe mamba unayelala ndani ya muto Nili! Wewe unafikiri kwamba muto Nili ni wako, kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!
Yesu akawajibu: “Watu wa kizazi kibaya na kinachokosa uaminifu mbele ya Mungu, wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataona kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha nabii Yona.
Lakini kama nikiyatenda, hata ikiwa hamuniamini mimi, basi mwamini matendo yangu, kusudi mupate kujua kabisa kwamba mimi na Baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu, nami ndani yake.”