na ninyi mupate kuwaelezea watoto wenu na wajukuu wenu jinsi nilivyowachekelea Wamisri kwa kuonyesha vitambulisho vile kati yao. Hivyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.”
Viongozi wa mufalme wakamwuliza: “Mutu huyu atatusumbua mpaka wakati gani? Uwaache watu hawa wajiendee wamutumikie Yawe, Mungu wao. Haujali kwamba inchi ya Misri inaangamia?”
Halafu mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye atawafuatilia. Nami nitajipatia utukufu kwa kumwangamiza yeye na jeshi lake. Halafu Wamisri watatambua kwamba mimi ni Yawe.” Basi, Waisraeli wakafanya hivyo.
Musa akamwelezea baba mukwe wake mambo yote Yawe aliyomutendea mufalme wa Misri na Wamisri kwa ajili ya Waisraeli. Akamwambia vilevile juu ya shida zote zilizowapata katika safari na jinsi Yawe alivyowaokoa.
Lakini Yawe akamujibu Musa: “Sasa utaona jinsi nitakavyomutendea mufalme wa Misri. Kwa nguvu atalazimishwa kuwaacha watu wangu watoke. Kwa nguvu atawafukuza waondoke katika inchi yake.”
Kwa hiyo, uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yawe! Mimi nitawatoa katika nira mulizowekewa na Wamisri. Nitawaokoa toka utumwa wenu. Nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuwaazibu vikali Wamisri na kuwakomboa ninyi.
Lakini Musa akamujibu: “Hapana! Haifai kufanya hivyo, maana sadaka tutakazomutolea Yawe, Mungu wetu, zitawachukiza Wamisri. Wamisri wakituona tunatoa sadaka ambazo ni chukizo kwao, si watatupiga mawe?
Sema hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Sidona, na kuonyesha utukufu wangu kati yako. Nitakapotimiza hukumu zangu juu yako na kukuonyesha utakatifu wangu, halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.
Nitalitakasa jina langu kubwa mulilokufuru kati ya mataifa. Na kwa hiyo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nitawatumia ninyi kuonyesha utakatifu wangu mbele yao.
Nitajulisha jina langu takatifu kwa watu wangu Waisraeli, wala sitaruhusu tena watu walikufuru jina langu takatifu. Nayo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe, Mutakatifu wa Israeli.