Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 7:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Lakini nitafanya moyo wa mufalme kuwa mugumu. Na hata kama nitazidisha vitambulisho na maajabu yangu katika inchi ya Misri,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 7:3
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ulifanya miujiza na maajabu mbele ya Mufalme wa Misri, watumishi wake wote na watu wote wa inchi yake; maana ulijua kwamba waliwagandamiza babu zetu. Ukajipatia utukufu unaokuwa mpaka leo.


Alifanya miujiza na maajabu kwako, ee Misri, mufalme wa Misri na wakubwa wake wote.


Alifanya maajabu mbele ya babu zao, katika mbuga za Soani kule Misri.


Basi, Musa na Haruni walifanya maajabu hayo yote mbele ya mufalme wa Misri. Lakini Yawe alifanya moyo wa mufalme kuwa mugumu, akakataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke katika inchi yake.


Yawe akamwambia Musa: “Mufalme wa Misri hatakusikiliza, kusudi maajabu yangu yapate kuongezeka katika inchi ya Misri.”


Halafu mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye atawafuatilia. Nami nitajipatia utukufu kwa kumwangamiza yeye na jeshi lake. Halafu Wamisri watatambua kwamba mimi ni Yawe.” Basi, Waisraeli wakafanya hivyo.


Kwa hiyo nitaunyoosha mukono wangu na kupiga inchi ya Misri kwa maajabu ambayo nitayafanya kule. Kisha mufalme atawaacha muondoke.


Yawe akamwambia Musa: “Utakapofika Misri, uhakikishe kwamba umetenda mbele ya mufalme wa Misri miujiza yote niliyokupa uwezo wa kuifanya. Lakini mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye hatawaachilia Waisraeli waondoke.


Kisha Musa na Haruni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa Waisraeli.


Kisha Mungu akamwambia: “Ingiza tena mukono wako kwenye kifua chako!” Musa akaingiza mukono wake kwenye kifua. Alipoutoa inje, ukarudilia hali yake ya kawaida kama vile mwili wake unavyokuwa.


Hata hivyo, moyo wa mufalme ulibaki tu kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza. Ikakuwa kama vile Yawe alivyosema.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Moyo wa mufalme ni kama maji yanayotiririka; Yawe anauongoza popote anapopenda.


Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?


Kama wakati ulipotutoa toka katika inchi ya Misri, utuonyeshe tena maajabu yako.


Basi Yesu akamwambia: “Ninyi hamuwezi kuamini hata kidogo kama musipoona vitambulisho na maajabu.”


“Ninyi wanainchi wenzangu Waisraeli, musikilize maneno haya: Yesu wa Nazareti alikuwa mutu aliyetambulishwa wazi na Mungu mbele yenu kwa njia ya vitambulisho, miujiza, na maajabu aliyofanya katikati yenu kama munavyojua ninyi wenyewe.


Yeye ndiye aliyewaongoza Waisraeli toka Misri akifanya maajabu na vitambulisho katika inchi ile, na kwenye bahari Nyekundu na katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.


kwa njia ya uwezo wa vitambulisho na maajabu, na kwa uwezo wa Roho Mutakatifu. Hivi tokea Yerusalema mpaka kufika katika jimbo la Iliriko nimehubiri fasi zote Habari Njema ya Kristo.


Basi ni kusema kwamba Mungu anamuhurumia yule anayetaka, na kumufanya mugumu yule anayetaka.


Kuna Mungu yeyote mwingine aliyejaribu hata kidogo kwenda kujitwalia taifa lake kutoka taifa lingine, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyofanya, kwa kutumia majaribio, vitambulisho, maajabu, vita, na vitisho? Hapana. Lakini mulishuhudia kwa macho yenu namna Yawe alivyofanya kwa mukono wake wenye nguvu kabisa kule Misri.


Mukumbuke ugonjwa mukali muliouona kwa macho yenu, miujiza na maajabu na nguvu kubwa na uwezo mukubwa, ambavyo Yawe, Mungu wenu alitumia kwa kuwakomboa; vile ndivyo atakavyowatendea watu munaowaogopa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ