Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 7:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Basi, mufalme wa Misri akarudi katika nyumba yake na hata yale yaliyotokea hakuyajali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 7:23
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mwanadamu ni nini hata umujali? Kwa nini unajishugulisha naye


Wanadamu wote ni kama pumzi tu; wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu. Wakipimwa wote pamoja, pumzi ni nzito kuliko wao.


Lakini wachawi wa Misri kwa kutumia uchawi wao wakafanya vivyo hivyo. Kwa hiyo moyo wa mufalme wa Misri ukabaki kuwa mugumu, naye hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Wamisri wote wakachimbachimba kandokando ya muto Nili kusudi wapate maji ya kunywa, maana hawakuweza kunywa maji ya muto ule.


Wakubwa wamoja wa mufalme wa Misri wakaogopa maneno hayo ya Yawe, wakawapeleka watumwa na nyama wao ndani ya nyumba pahali pa usalama.


Lakini yule ambaye hakujali neno la Yawe aliwaacha watumwa wake na nyama wake katika mashamba.


Tega sikio usikie maneno ya wenye hekima; elekeza moyo wako kwa maarifa yangu.


Niliangalia, nikawaza. Kwa mwisho nikapata fundisho:


Heri mutu anayemwogopa Yawe siku zote, lakini mwenye moyo mugumu atapata hasara.


Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Ulijisemesha ndani ya moyo: “Nitakuwa malkia milele”, nawe haukufikiri juu ya mambo yanayotokea, wala kuwaza juu ya mwisho wake.


Lakini, ingawa mufalme na watumishi wake wote waliyasikia maneno hayo yote, hawakuogopa wala kurarua nguo zao kwa huzuni.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Basi, akaniambia hivi: Wewe mwanadamu! Angalia vizuri na kusikiliza kwa uangalifu. Shika kwa moyo uone kila kitu nitakachokuonyesha maana umeletwa hapa kusudi nikuonyeshe kitu. Unapaswa kuwatangazia watu wa Israeli kila kitu utakachoona.


Mungu akasema: Muangalie mataifa, muone! Mustaajabu na kushangaa. Maana ninatenda kitu ukiwa bado unaishi, kitu ambacho ungeambiwa haungesadiki.


Ni lazima muniheshimu mimi kwa matendo yenu. Musiponisikiliza nitawaletea laana. Vitu vyote munavyopewa kwa mahitaji yenu nitavilaani. Na kweli nimekwisha kuvilaani, kwa sababu hamushuguliki hata kidogo na maagizo yangu.


akawaambia: “Muweke ndani ya mioyo yenu maneno yote ambayo ninawapa leo. Muwaamuru watoto wenu kusudi wafuate kwa uaminifu maneno yote ya sheria hii.


Basi, kwa sababu alikuwa karibu ya kufa, wanawake waliokuwa wanamuzalisha walimwambia: “Usiogope, maana umezaa mutoto mwanaume.” Lakini yeye hakujibu neno, wala hakuwasikiliza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ