Musa na Haruni wakafanya kama vile Yawe alivyowaamuru. Haruni akainua fimbo yake juu mbele ya mufalme wa Misri na wakubwa wake, akayapiga maji ya muto Nili, na maji yote katika muto yakageuka kuwa damu.
Lakini wachawi wa Misri kwa kutumia uchawi wao wakafanya vivyo hivyo. Kwa hiyo moyo wa mufalme wa Misri ukabaki kuwa mugumu, naye hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.