Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 7:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Musa na Haruni wakafanya kama vile Yawe alivyowaamuru. Haruni akainua fimbo yake juu mbele ya mufalme wa Misri na wakubwa wake, akayapiga maji ya muto Nili, na maji yote katika muto yakageuka kuwa damu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 7:20
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Elisha akamwambia Gehazi: “Ujitayarishe kusafiri, twaa fimbo yangu, na uende mara moja. Usisimame katika njia kwa kumusalimia mutu yeyote, na mutu yeyote akikusalimia katika njia, usipoteze wakati kwa kumurudishia salamu. Kwenda moja kwa moja mpaka katika nyumba na kuweka fimbo yangu juu ya uso wa mutoto.”


Akageuza mito yao kuwa damu, akaua samaki wao wote.


Aligeuza ile mito kuwa damu, Wamisri wasipate maji ya kunywa.


Lakini wasipoamini hata vitambulisho hivi viwili, au kuamini maneno yako, utachota maji ya muto Nili na kuyamwanga juu ya inchi kavu. Maji hayo yatakuwa damu juu ya inchi kavu.”


Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kufanya kama vile walivyoamuriwa na Yawe. Haruni akatupa fimbo yake chini mbele ya mufalme na wakubwa wake, nayo ikakuwa nyoka.


Samaki wakakufa, muto ukanuka vibaya sana hata Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Inchi nzima ikajaa damu.


Basi, Musa na Haruni wakafanya hivyo. Hakika, walifanya kama vile Yawe alivyowaamuru.


Ee Yawe, umeikasirikia mito? Umeyakasirikia maji ya bahari? Ulipanda juu ya gari lako la vita na kuendesha farasi kwa kupata ushindi.


Kisha malaika wa pili akapiga baragumu. Halafu kitu kimoja chenye kufanana na mulima mukubwa unaowaka moto kikatupwa katika bahari, na sehemu moja ya tatu ya bahari ikageuka damu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ