Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 7:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Basi, Yawe anasema kwamba sasa utamutambua yeye ni nani. Nitayapiga maji ya muto Nili kwa fimbo hii na maji yote yatageuka kuwa damu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 7:17
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu, mutu mumoja wa Mungu akamukaribia mufalme wa Israeli, akamwambia: “Yawe anasema hivi: ‘Kwa sababu Waaramu wamesema kwamba mimi Yawe ni Mungu wa milima wala si Mungu wa inchi ya bonde, nitakupa ushindi juu ya kundi hili kubwa, nawe utatambua kwamba mimi ni Yawe.’ ”


Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe tu, ee Yawe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”


Akageuza mito yao kuwa damu, akaua samaki wao wote.


Aligeuza ile mito kuwa damu, Wamisri wasipate maji ya kunywa.


Wafezeheke na kuhangaika milele, waangamie kwa haya kabisa.


Mataifa yameanguka katika shimo walilochimba, miguu yao imenaswa kwenye wavu waliotega.


Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.”


na ninyi mupate kuwaelezea watoto wenu na wajukuu wenu jinsi nilivyowachekelea Wamisri kwa kuonyesha vitambulisho vile kati yao. Hivyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.”


Lakini wasipoamini hata vitambulisho hivi viwili, au kuamini maneno yako, utachota maji ya muto Nili na kuyamwanga juu ya inchi kavu. Maji hayo yatakuwa damu juu ya inchi kavu.”


Lakini mufalme wa Misri akawauliza: “Ni nani yule Yawe, hata nimusikilize na kuwaacha Waisraeli waondoke? Mimi simujui yule Yawe, wala sitawaruhusu Waisraeli waondoke.”


Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Musa na Haruni wakafanya kama vile Yawe alivyowaamuru. Haruni akainua fimbo yake juu mbele ya mufalme wa Misri na wakubwa wake, akayapiga maji ya muto Nili, na maji yote katika muto yakageuka kuwa damu.


wakati nitakaponyoosha mukono wangu juu ya inchi ya Misri na kuwatoa Waisraeli kati yao. Halafu Wamisri watatambua kwamba mimi ni Yawe.”


Nitawalipiza kisasi kikali kwa azabu ya kasirani. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Kwa sababu umesema kwamba muto Nili ni wako, kwamba ndiwe uliyeufanya, basi, inchi yako, Misri, itakuwa tupu na jangwa. Halafu watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Ndivyo nitakavyoiazibu Misri. Na watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitakapoiteketeza Misri kwa moto na kuvunjavunja wasaidizi wake wote, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitakapoifanya inchi ya Misri kuwa jangwa na mali yake yote kunyanganywa, nitakapowaua wakaaji wake wote, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitaikunywesha inchi damu yako mpaka juu ya milima, mashimo yatajaa damu yako.


Ndivyo nitakavyofanya kusudi yote yaone ukubwa wangu na utakatifu wangu. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Kisha watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao, kwa sababu mimi niliwapeleka katika uhamisho kati ya mataifa na kuwarudisha tena katika inchi yao. Sitamwacha hata mutu wao mumoja abakie kati ya mataifa.


Muti uliouona ukiwa mukubwa na wenye nguvu, ambao matawi yake marefu yalifika mbinguni, nao ukionekana kutoka kila pahali katika dunia,


Wakaaji wote wa dunia si kitu; anafanya anavyotaka na viumbe vya mbinguni, na wakaaji wa dunia; hakuna anayeweza kumupinga, au kusema: Unafanya nini?


Alifukuzwa mbali na wanadamu, akili yake ikafanywa kama ya nyama, akaishi na punda wa pori, akakuwa anakula majani kama ngombe, na kulowanishwa na umande wa mbinguni mpaka alipotambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Nao wako na uwezo wa kufunga mbingu kusudi mvua isinyeshe wakati wanapotangaza ujumbe wa Mungu. Wako vilevile na uwezo wa kugeuza maji kuwa damu, na uwezo wa kuleta mapigo ya kila namna kila wakati wanapotaka.


Kisha malaika wa pili akapiga baragumu. Halafu kitu kimoja chenye kufanana na mulima mukubwa unaowaka moto kikatupwa katika bahari, na sehemu moja ya tatu ya bahari ikageuka damu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ