Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 7:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kisha umwambie hivi: Yawe, Mungu wa Waebrania, amenituma kwako, naye anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waende zao kusudi wanitumikie katika jangwa. Lakini mpaka sasa wewe haupendi kutii.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 7:16
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Mufalme wa Misri kwa ugumu wake alikataa kutuachilia tuondoke. Kwa hiyo Yawe akamwua kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri, muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu na wa nyama. Basi, mimi ninamutolea Yawe sadaka kila muzaliwa wa kwanza dume wa mifugo yangu. Lakini kila muzaliwa wa kwanza wa wana wangu ninamukomboa.’


Mufalme wa Misri aliposikia kwamba Waisraeli wamekimbia, yeye na wakubwa wake walibadilisha mafikiri yao, wakasema: “Tumefanya nini kwa kuwaachilia Waisraeli waende zao wasitutumikie tena?”


Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”


Halafu, Musa akamwambia Mungu: “Sasa, nikiwaendea Waisraeli na kuwaambia: ‘Mungu wa babu zenu amenituma kwenu’, nao wakiniuliza: ‘Jina lake ni nani?’, nitawaambia nini?”


“Wao watakusikiliza, nawe pamoja na wazee wa Waisraeli mutamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: ‘Yawe, Mungu wa Waebrania, ametutokea. Sasa, uturuhusu tuende safari ya mwendo wa siku tatu katika jangwa, tumutolee Yawe, Mungu wetu, sadaka.’


Nawe utamwambia mufalme wa Misri kwamba Yawe anasema hivi: ‘Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.


Nami ninakuambia: Umwache mwana wangu aondoke, kusudi anitumikie! Kama ukikataa kumwachilia aondoke, angalia nitamwua muzaliwa wako wa kwanza mwanaume.’ ”


Mufalme wa Misri hatakusikiliza. Na hapo nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuazibu vikali inchi ya Misri na kuwatoa watu wangu, makabila ya Israeli, kutoka Misri. Nitafanya hivyo kwa matendo makubwa ya hukumu juu ya Misri,


Yawe akamwambia Musa: “Umwambie Haruni anyooshe mukono wake na kuinua fimbo yake juu ya mito, juu ya mifereji na visima, nao vyura watatokea na kuenea kila pahali katika inchi ya Misri.”


Yawe akafanya kama vile alivyosema. Makundi makubwa ya mainzi yakashambulia nyumba ya mufalme wa Misri, nyumba za wakubwa wake na inchi nzima ya Misri. Inchi nzima ya Misri ikaharibiwa na mainzi wale.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa mufalme wa Misri umwambie kwamba mimi Yawe, Mungu wa Waebrania, ninasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Kisha, Yawe akamwambia Musa: “Kesho, amuka asubui mapema umwendee mufalme wa Misri, umwambie kwamba mimi Yawe, Mungu wa Waebrania, ninasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Ni mimi niliyemwamuru Kiro akuje, atimize mapenzi yangu. Nitazifanikisha njia zake zote. Ataujenga upya muji wangu Yerusalema, na kuwapa uhuru watu wangu wanaokuwa katika uhamisho, bila kutaka malipo wala zawadi. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Watu wa Israeli wanagandamizwa pamoja na watu wa Yuda. Wale waliokamata mateka wamewabana sana na wanakataa kuwaachilia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ