Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 7:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kisha Yawe akamwambia Musa: “Moyo wa mufalme wa Misri umekuwa mugumu. Anakataa kuwaacha Waisraeli waondoke.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 7:14
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa mufalme wa Misri. Mimi nimefanya moyo wake kuwa mugumu na wa wakubwa wake kusudi nipate kuonyesha vitambulisho hivi kati yao,


Lakini Yawe akafanya moyo wa mufalme kuwa mugumu, naye hakuwaachilia Waisraeli waondoke.


Lakini Yawe akaufanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, akakataa kuwaachilia Waisraeli waondoke.


Ukikataa kuwaacha watu wangu waondoke, basi, kesho nitaleta nzige washambulie inchi yako.


Ninajua kwamba mufalme wa Misri hatawaacha muende asipolazimishwa kwa mukono wenye nguvu.


Nami ninakuambia: Umwache mwana wangu aondoke, kusudi anitumikie! Kama ukikataa kumwachilia aondoke, angalia nitamwua muzaliwa wako wa kwanza mwanaume.’ ”


Hata hivyo, moyo wa mufalme ulibaki tu kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza. Ikakuwa kama vile Yawe alivyosema.


Basi, kwenda ukutane naye kesho asubui, wakati anapokwenda kwenye muto Nili. Umungojee kando ya muto. Utwae katika mukono wako ile fimbo iliyogeuka kuwa nyoka.


Lakini mufalme wa Misri alipoona kwamba inchi imepata utulivu, akakuwa na moyo mugumu tena, wala hakusikiliza Musa na Haruni, kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Wale wachawi wakamwambia mufalme wa Misri: “Hii ni kazi ya mukono wa Mungu.” Lakini moyo wa mufalme ukaendelea kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Basi, Haruni akainua fimbo yake juu ya maji yote. Vyura wakatokea na kufunika inchi nzima ya Misri.


Kama ukikataa kuwaacha waondoke na ukiendelea kuwashikilia,


Lakini mufalme wa Misri alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo vimekoma, akarudilia zambi yake tena. Akafanya moyo wake kuwa mugumu, yeye pamoja na wakubwa wake.


Mufalme wa Misri akauliza habari juu ya nyama wa Waisraeli. Wakamwambia kwamba hakuna nyama wao hata mumoja aliyekufa. Hata hivyo, Mufalme akabaki akifanya moyo wake kuwa mugumu, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.


Lakini mukikataa na kuniasi, mutaangamizwa kwa upanga. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Mbona basi, watu hawa wameacha njia inayokuwa sawa na kuendelea katika upotovu wao? Wanashikamana na miungu yao ya uongo, na kukataa kunirudilia mimi!


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitawasafisha na kuwapima kwa moto kama vile chuma. Ni namna gani zaidi ya kuwatendea hawa watu wangu waovu?


Wakaifanya mioyo yao kuwa migumu kama jiwe, wasipate kusikia sheria yangu mimi Yawe wa majeshi niliyoitangaza kwa roho yangu kwa kupitia manabii waliotangulia. Kwa hiyo, mimi Yawe wa majeshi nikawaka hasira juu yao,


“Lakini Sihoni, mufalme wa Hesiboni, hakuturuhusu tupite katika inchi yake. Yawe, Mungu wenu, akamufanya akuwe na kichwa kigumu na mugumu wa moyo, kusudi tumushinde na kutwaa inchi yake ambayo tunairizi mpaka leo.


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Kwa nini munafanya mioyo yenu kuwa migumu kama Wamisri na Mufalme wao? Mungu alipowachekelea Wamisri, hawakuwaacha Waisraeli waondoke, nao wakaondoka?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ