12 Kila mumoja akatupa fimbo yake chini, ikakuwa nyoka. Lakini fimbo ya Haruni ikameza fimbo zao.
Lakini, mufalme wa Misri akawaita wenye hekima wake na wachawi. Wale wachawi wa Misri wakafanya vile vile kwa uchawi wao.
Hata hivyo, moyo wa mufalme ulibaki tu kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza. Ikakuwa kama vile Yawe alivyosema.
Hata wale wachawi hawakuweza kujitokeza, maana wao pamoja na Wamisri wote vilevile walipatwa na majipu hayo.
Lakini hawataendelea mbali sana, kwa sababu upumbafu wao utaonekana wazi mbele ya watu wote, sawa ilivyokuwa kwa Yane na Yambure.
Lakini ninyi, watoto wangu, muko watoto wa Mungu, nanyi mumewashinda manabii wa uongo; maana roho anayekaa ndani yenu ni mwenye uwezo kuliko yule anayekaa ndani ya watu wa dunia.